Wednesday 13 November 2013

Wakenya tupo katika majuto


 


Rais Uhuru Kenyatta akiwapungia wananchi wa Kenya siku ya kuapishwa kwake mapema mwaka huu. 
Na Dorothy Jebet,Mwananchi

Posted  Jumatano,Novemba13  2013  saa 13:8 PM
Kwa ufupi
Upinzani umegundua kwamba Serikali ya Jubilee imeanza kuonyesha kucha zake miezi michache baada ya kujifanya kwamba inafuata sheria na kulinda Katiba. Ilifanya hivyo kwa kuteua Baraza la Mawaziri inavyotakiwa kisheria, lakini sasa mambo yamebadilika.

“Tulionywa na Amerika kabla ya uchaguzi kwamba tukiwachagua Uhuru na Ruto tungejuta na sasa tumejuta. Wakenya milioni sita walimchagua Uhuru. Kweli sikio la kufa halisikii dawa.
Dalili ya mvua ni mawingu. Mawingu yanayofunika anga la Kenya wakati huu yanaashiria kwamba mvua itakayonyesha itasababisha mafuriko katika nyanja za kisiasa na kiuchumi.
Ni kwa sababu hii wote wanaojali hatima ya nchi hawana budi kujitokeza kimasomaso ili kuona athari za vitendo vya Serikali ya Jubilee kwa nchi na kutafuta jinsi ya kuepukana nazo.
Jukumu hili liko juu ya mabega ya vyama vya upinzani haswa Muungano wa CORD unaoongozwa na aliyekuwa Waziri Mkuu, Raila Odinga, Kalonzo Musyoka na wengine.
Ni wakati wa CORD kuonyesha kuwa haiwezi kusita kueleza na kuihakiki Serikali ya Uhuru Kenyatta pia ni dhabiti na kwamba viongozi wake watakuwa wanazungumza kwa sauti moja wanapoikosoa Serikali.
Wengi walitarajia kwamba viongozi wa Cord wangetengana baada ya uchaguzi mkuu, lakini Raila, Kalonzo Musyoka na Moses Wetangula bado ni wanachama wa CORD.
Historia ya vyama vya kisiasa nchini inaonyesha kwamba, viongozi huunda vyama kwa lengo la kushinda uchaguzi lakini baada ya miezi michache vyama hivyo husambaratika.
Kwa mfano, kiongozi wa United Democratic From (UDF), Musalia Mudavadi anajitayarisha kujiunga na Serikali ya Uhuru kama waziri. Gazeti moja la kila siku limenukuliwa likiripoti kwamba, Mudavadi hivi karibuni ataingizwa kwenye serikali.
Tatizo nini?
Upinzani umegundua kwamba Serikali ya Jubilee imeanza kuonyesha kucha zake miezi michache baada ya kujifanya kwamba inafuata sheria na kulinda Katiba. Ilifanya hivyo kwa kuteua Baraza la Mawaziri inavyotakiwa kisheria, lakini sasa mambo yamebadilika.
Uhuru na Makamu wake,William Ruto, wameonyesha kuwa hawajali lolote zuri linaloiweka Kenya kwenye jukwaa la mataifa yanayowalinda wananchi wake. Kwa wiki moja iliyopita, Upande wa Serikali bungeni umepitisha miswada miwili inayorudisha nyuma hatua nzuri zilizokuwa zimepigwa.
Kumekuwa na kilio kikuu kutoka kwa Wakenya kuhusu hatua ya Serikali kutaka kuzima uhuru wa wanahabari na pia kukata msaada kwa mashirika yasiyo ya kiserikali kutoka kwa mashirika ya maendeleo ya nchi za Ulaya na Magharibi.

Endelea kusoma habari hii: mwananchi