Sunday 10 November 2013

Msimamo wa Tanzania kutojitoa EAC wapongezwa na Kenya

 
 
 Siku chache baada ya rais wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania kutoa msimamo wa Tanzania kutokujitoa katika jumuiya ya Afrika mashariki waziri wa mambo ya nje wa Kenya amempongeza rais Jakaya Kikwete na kusema kuwa hatua hiyo itaimarisha zaidi uhusiano wa juimuiya hiyo.
Kauli hiyo imekuja siku tatu baada ya raisi wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania kulihutubia bunge na kueleza msimamo huo ambapo waziri wa mambo ya nje wa Kenya Mh. Amina Mohamed aliekuja Tanzania kwa lengo la kumpongeza raisi amesema nchi yake imekuwa ikufanya baadhi ya maamuzi yanayohusu jumuiya bila kuishirikisha Tanzania kwa kutokujua wanakiukwaji taratibu za jumuiya na kwamba kunzaia sasa watafuata taratibu zote ili kuhakikisha jumuiya hiyo haitavunjika pamoja na uhusiano baina nchi uwanachama.
Kwa upande wake waziri wa mambo ya nje na ushirikiano wa kimataifa wa Tanzania Mh. Bernadi Membe mbali na kupongeza hatua ya waziri wa Kenya amefafanua msimamo wa Tanzania kuhusu swala la ardhi pamoja na shirikisho la haraka katika jumuiya ya Afrika mashariki utaendelea kuwa palepale na kuwa swala la shirikisho linahitaji muda wa kujadiliwa ili kila nchi uanachama waweze kujiridhisha.
 Wakati huo huo mwenyekiti wa chama cha wananchi -CUF Profesa Ibrahimu Lipumba amesema hatua ya raisi Kikwete ni ya kizalendo na kwamba kuna haja ya wachambuzi wa mambo ya uhusiano wa kimataifa kuchambua kwa kina ili kubaini chanzo cha tatizo lililojitokeza katika jumuiya hiyo ili kuhakikisha haitatokea tena na uhusiano baina ya nchi uanachama unaimarika. 

SOURCE; ITV