Saturday 9 November 2013

Exhibitionism: Magonjwa ya akili ya ngono yanayosumbua Watanzania wengi

“Kwa kitaalamu, ugonjwa wa akili ya ngono wa kupenda kuacha mwili wazi  unaitwa ‘exhibitionism’ ambapo mtu huweza kuamua kuacha maziwa, mapaja au kwa wanaume kuvaa suruali inayoelekea kuanguka kutoka maungoni,” Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Akili na mtaalamu wa waathirika wa dawa za kulevya, Augustine Godman 
Na  Florence Majani, Mwananchi

Posted  Ijumaa,Novemba8  2013  saa 10:40 AM
Kwa ufupi
  • Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Akili na mtaalamu wa waathirika wa dawa za kulevya, Augustine Godman anasema, magonjwa ya akili kwa ujumla wake yanaweza kuzidi 1,886 lakini yapo yale ya ngono ambayo pengine yana changamoto lukuki kwa mwanadamu hasa Watanzania wasiofahamu kuwa ni magonjwa ya akili.


Huenda tumewaona wengi wao kama mashujaa, vijana wa kisasa au hata dada zetu wanaokwenda na wakati, kumbe ni wagonjwa wa akili.
Unasikiliza taarifa ya habari jioni. Unasikia kuwa, mwanamume amembaka mtoto wa miezi mitatu. Unaihoji nafsi yako… ni jambo gani lililosababisha akafanya ukatili huo? Je, ni tamaa kali ya ngono?
Wengine hudhani ni kisasi au imani za kishirikina na kwamba wahusika wametumwa.
Huu ni upotoshaji, lakini ukweli ni kuwa hayo ni magonjwa ya akili ya ngono ambayo yanawakumba asilimia 35 au zaidi ya Watanzania wote.
Watanzania hawa wanaugua magonjwa haya kwa wakati mmoja na kusababisha madhara mbalimbali kijamii, kiuchumi na migogoro katika familia na katika uhusiano.
Watu wenye magonjwa haya, si lazima watembee wakiokota makopo, kuvua nguo au kuwa na nywele ambazo hazijachanwa.
Hawa ni watu wa kawaida ambao tunafanya nao kazi, wenye uwezo mkubwa katika taaluma au pengine ni wazazi au hata walezi.
Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Akili na mtaalamu wa waathirika wa dawa za kulevya, Augustine Godman anasema, magonjwa ya akili kwa ujumla wake yanaweza kuzidi 1,886 lakini yapo yale ya ngono ambayo pengine yana changamoto lukuki kwa mwanadamu hasa Watanzania wasiofahamu kuwa ni magonjwa ya akili.
Dk Godman anafafanua kuwa magonjwa ya akili ya ngono  kuwa ni yale yanayohusisha athari , upungufu  au mparaganyiko au  vitu visivyo vya kawaida  katika tendo la ngono.
“Mtu anaweza kuwa na  matatizo ya kihisia au ya kisaikolojia au vya kitabia katika  suala la ngono na huweza kusababisha madhara au kutopata mafanikio,” anasema Dk Godman
Daktari huyu ambaye amewahi pia kufundisha Chuo Kikuu cha Sayansi ya Tiba Muhimbili (Muhas), kitengo cha magonjwa ya akili anasema  watu wengi wana magonjwa ya akili ya ngono, lakini hawajui kama ni magonjwa  na wanaendelea kuishi hivyo hivyo wakidhani ndivyo walivyo na baadhi wakipata matatizo katika jamii, wengine kufungwa jela au kupigwa kutokana na tabia hizo.
Mara nyingi tumekuwa tukiona wanawake wanavaa mavazi ya nusu uchi, wakizianika  nje sehemu kubwa za miili yao.

Tabia hizo ambazo  pengine huweza kuigwa na wengine  ni miongoni mwa magonjwa ya akili ya ngono kwani watu wanaopenda kufanya hivyo hujisikia raha na amani watu baki au wageni wenye jinsi tofauti wanapoyaangalia maungo yao na kushtuka.
“Kwa kitaalamu, ugonjwa wa akili ya ngono wa kupenda kuacha mwili wazi  unaitwa ‘exhibitionism’ ambapo mtu huweza kuamua kuacha maziwa, mapaja au kwa wanaume kuvaa suruali inayoelekea kuanguka kutoka maungoni,” anasema
Anasema, watu aina hii hutosheka kimapenzi mara tu wanapoona wanaume au wanawake wengine wameyaona maungo yao.  Hata hivyo, anasisitiza kuwa hutosheka pale tu watu wageni wanapoyaona maungo yao.
Mhadhiri wa Sosiolojia, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dk Thomas Ndaluka anasema, baadhi ya magonjwa haya yanasababishwa na historia ya mtu.
Anasema hata hivyo mparaganyiko kama ule wa kupenda kuacha maungo wazi, unaambukiza kwa maana ya kuwa, anayeanza kufanya hivyo ni mgonjwa wa akili na matokeo yake wengine wanaiga.
Ubakaji wa watoto wachanga
Wengi wamekuwa wakihusisha ugonjwa huu na imani za kishirikiana, lakini ukweli ni kuwa, wale wanaowabaka watoto wadogo au kuwalawiti wana matatizo ya akili ambayo kitaalamu yanaitwa pedophilia (paedophilia).
“Katika hali ya kawaida si rahisi mtu mzima akamtamani kimapenzi mtoto wa miezi mitatu,” anasema mtaalamu huyo.
Ugonjwa huu unatokea pale mtu anapokuwa na hali ya kupata raha ya ngono kwa watoto wadogo wenye umri wa chini ya miaka mitano.
“Watoto wa jinsi zote huweza kuathiriwa na tatizo hili. Mtu mwenye ugonjwa huu huweza kuamua kumuingilia mtoto au tu kuamua kumchezea via vyake vya uzazi,” anasema Dk Godman.
Mhadhiri wa Saikolojia, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Dk Kitila Mkumbo anasema sababu kuu za maradhi hayo ya akili ni pamoja na mazingira ya mtu wakati wa balehe, aliambiwa nini kuhusu tendo la ndoa na makuzi yake kwa jumla.

“Kwa mfano  inategemea kijana anaambiwa nini wakati wa balehe au yeye mwenyewe anaelewa nini maana ya tendo hilo” anaeleza Dk Mkumbo.
Anatoa mfano kuwa, wapo baadhi ya wanaume wanaamini au kufananisha kila shimo na uke.
“Huu ni ugonjwa mkubwa sana. Ndiyo maana utasikia mtu kambaka mbuzi. Yeye anaamini kila shimo linaweza kutumika kama uke”, anasema
Anafafanua kuwa magonjwa mengi ya akili ya ngono hujitokeza wakati wa balehe  na hukua kadri mtu anavyokosa matibabu.
Yapo matukio kadhaa yaliyowahi kutokea hapa nchini yanayoeleza watu waliowabaka watoto wadogo.
Kwa mfano, Desemba 2012, Yakobo Raymond alifikishwa mahakamani huko wilayani Muheza, Mkoani Tanga kwa tuhuma za kumbaka mtoto wake wa  kambo mwenye umri wa miaka mitatu.
Pia, huko mkoani Arusha, mwezi Januari mwaka jana, David  Samweli mkazi wa Moivaro Wilaya ya Arumeru, aliwabaka watoto wawili wa kike wa jirani yake na mtoto wake  wa kumzaa kwa nyakati tofauti chumbani kwake.
Licha ya matukio  kama haya kuripotiwa zaidi kwa wanaume wenye tabia hii, Dk Godman anasema wapo wanawake ambao pia huwabaka watoto wadogo wa kiume.
“Mwanamke anaweza kumvua nguo mtoto mdogo na kuanza kumshikashika tu, hapo huwa amepata  raha yake. Lakini pia anaweza kuamua kumwacha mtoto akiwa uchi,” anasema
Mtu mwenye ugonjwa huu humrubuni mtoto kwa vitu vidogo vidogo ili ampende na kumweka karibu naye na wakati mwingine baada ya kumfanyia vitendo hivyo humtishia kuwa akisema, atamdhuru.
 Tafiti mbalimbali zinaeleza kuwa, wapo watu katika nchi zilizoendelea ambao huasili  watoto, kisha kuwatendea vitendo hivi vya upedofilia................................

Endelea kusoma habari hii:  mwananchi