Monday 28 October 2013

Watu 2 wanatuhumiwa kwa ugaidi wauawa Kilindi -Tanga





 Watu wawili wanaodaiwa kuhusishwa na vitendo vya kigaidi wameuawa kwa kupigwa risasi wakati kundi hilo lilipokuwa msikitini huku wafuasi wake wakiwa na silaha za moto na baridi walipokuwa wakijibizana kwa kutumia silaha mbali mbali ndipo askari walipowahi kuwashambulia viongozi wa kundi hilo kisha kuwanyang'anya silaha zao ili kuepuka madhara makubwa zaidi.

Mkuu wa mkoa wa Tanga luteni mstaafu Chiku Gallawa amesema tukio hilo limetokea katika kijiji cha Kimamba kilichopo kata ya Negero wilayani Kilindi wakati kundi hilo lilipokuwa limejiandaa kujibu mashambulizi ya askari msikitini kwa kuwa na silaha aina ya bunduki na mapanga ndipo viongozi hao waliposhambuliwa ambapo mmoja alifariki papo hapo huku mwingine akifariki hospitali ya wilaya.


SOURCE: ITV