Monday 28 October 2013

Mbivu au mbichi kwa Ntagazwa leo


Na Tausi Ally, Mwananchi

Posted  Jumatatu,Oktoba28  2013  saa 10:34 AM
Kwa ufupi
Ni wakati hukumu katika kesi yake ya tuhuma za utapeli, itakapotolewa mahakamani.


Dar es Salaam.  Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam,  leo  itatoa hukumu kuhusu  kesi  ya utapeli inayomkabili mwanasiasa mkongwe, Arcado Ntagazwa na wenzake wawili.
Ntagazwa aliwahi kuwa waziri wa Serikali. Hukumu hiyo imeahirishwa mara mbili, mara ya kwanza ilikuwa Oktoba 17,mwaka huu ambapo Hakimu Mkazi Geni Dudu, alisema alikuwa bado anaiandika.
Mara ya pili ilikuwa Ijumaa iliyopita ambapo hakimu huyo alisema alikuwa anaihakiki hukumu.
 Siku hiyo ya Ijumaa Ntagazwa, alifika  mahakama saa 2.00 asubuhi akionekana mwenye kujiamini.
Alioonekana akiongea na waandishi  wa habari nje ya mahakama na baadaye kupiga nao picha  kabla ya kwenda mahakamani kusikiliza hatima yake.
Ntagazwa,  mwanaye  Webhale Ntagazwa na  mshirika wake, Senator Miselya (60), wanakabiliwa na kesi  ya utapeli kwa  kujipatia kwa njia ya udanganyifu, fulana 5,000 na kofia idadi kama hiyo  za kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere.
Sare hizo zinadaiwa kuwa na thamani ya Sh 74,950,000, mali ya Noel Severe.
Wakati wa usikilizaji wa awali wa kesi hiyo, Ntagazwa  alikanusha madai dhidi yake.
Hata hivyo katika ushahidi wake wa utetezi, mshtakiwa  alikubali  kuwa alikuwa hajalipa   Sh 74, 950,000 kwa ajili ya vifaa hivyo.
Pia alidai kuwa aliwadanganya polisi  kwa  kukubali shtaka hilo mbele yao.
Alidai kuwa alikubali shtaka hilo ili kukwepa kusumbuliwa.
Washtakiwa katika kesi hiyo pia walikubali kupokea fulana na kofia  lakini walirushiana  mpira  kuhusu  malipo ya fedha  hizo.

Washtakiwa hao walilazimika kupanda kizimbani kujitetea baada ya mahakama kuwaona kuwa wana kesi ya kujibu.
Upande wa mashtaka uliwaita mashahidi watano.
Washtakiwa katika kesi hiyo, wanadaiwa kutenda makosa hayo Oktoba 24, 2009, katika maeneo ya Mikoroshini.
Inadaiwa kuwa   walimuahidi Severe kwamba wangemlipa kiasi hicho cha fedha ndani ya mwezi mmoja huku wakijua
SOURCE: MWANANCHI