Toka jana jioni wakazi wa jiji la Arusha wameendelea kuwa katika taharuki na minong'ono hapa na pale kutokana na tukio la kupigwa risasi binti mmoja aitwaye Violeth Mathias katika ofisi za TRA Arusha.

Mwanadada huyu aliyeonesha jeuri ambayo haikutegemea si tu Arusha bali katika Taifa hili hasa lile la kwenda na kuchukua Bastola na kutaka kummaliza askari aliyekuwa akitimiza wajibu wake katika Bank ya CRDB. Kitendo hiki kimelfanya wakazi wa jiji hili kuwa na Maswali mengi kuliko majibu. Hasa juu ya anakota jeuri ama kiburi mwanadada huyu.