Saturday 31 August 2013

Somalia yakaribisha TED-X


 31 Agosti, 2013 - Saa 13:30 GMT

                            Barabara ya Mogadishu
Wasomi, wasanii na wafanya-biashara wa Somalia wamekuwa wakizungumza katika mji mkuu, Mogadishu, kwenye ile mikutano inayofanywa sehemu mbali-mbali za dunia iitwayo TED-EX.
Mazungumzo hayo yaliyofanywa kwenye ukumbi wa mikutano chini ya ulinzi mkubwa, yalihusu mapendekezo na ubunifu wa kuijenga tena Somalia.
Hotuba katika vikao vya TED-EX zimetolewa katika nchi zaidi ya 150.

source: BBC Swahili