Thursday 27 September 2012

MATUKIO KATIKA PICHA KUHUSU SIKU YA KUWAAGA WANATASAO WALIOMALIZA VYUO MBALIMBALI OSLO NA HAMAR 12.06.2012

Saturday 22 September 2012

 Mhe Rais Godrick Lyimo kulia, katikati ni rais mstaafu Mhe Doreen Ndosi na kushutu ni Mchg Eilzabeth Silayo mwanafunzi Oslo University


KUHUSU KUWAKARIBISHA WANAFUNZI WAPYA KATIKA CHAMA CHA TASAO(TANZANIA STUDENT ASSOCIATION IN OSLO)

Tarehe 22/08/2012 jumuyia ya wanafunzi wa Tanzania wanaosoma Oslo, Norway wamekuta na kuwakaribisha wanafunzi wapya waliokuja kusoma shahada mbalimbali.

Mhe Rais wa TASAO Mchg. Godrick Lyimo alichakuwa nafasi ya kuwakaribisha wanafunzi hao waliokuja masomoni mwaka huu wa wa masaomo 2012/13. Mhe. Rais aliwapongeza sana wanafunzi hao kwa kupata nafasi ya kuja kusoma Norway, nafasi ambayo sio kila mtu anapata, Mhe Rais pia aliwaambia wanafunzi wapya malengo na madhumuni ya kuwepo kwa chama cha TASAO kuwa ni kujenga umoja wa wanafunzi wa Kitanzania ili waweze kusaidiana wakati wa shida na wa raha, kukaa kama ndugu wakiwa nje ya nchi yao. Mhe Rais aliwaomba wanafunzi wote wapya na wa zamani waendelee kushikamana na kusaidiana kama ndugu maana Tanzania ni moja na watu wake ni wamoja.